KILIMO BORA CHA VIAZI VITAMU

Related image

Viazi vitamu ni moja kati ya mazao makuu ya mizizi nchini Tanzania ambayo hulimwa kwa ajili ya chakula. Zao hili ni moja kati ya mazao ya kinga ya njaa kutokana na sifa yake ya kuvumilia ukame.

Zao la viazi vitamu, asilia yake ni Amerika ya Kati na ya Kusini. Nchini Tanzania, zao hili hulimwa zaidi katika mikoa ya Mara, Mwanza, Shinyanga, Dodoma, Morogoro, Kagera, Arusha na Ruvuma.

Matumizi
Viazi vitamu hutumika kama chakula kwa kutayarishwa katika njia mbalimbali kama
vichembe, na Matobolwa. Pia Unga wa viazi vitamu hutumika kutengeneza vyakula kama keki, maandazi, kalimati na tambi. Majani ya viazi huliwa kama mboga pia hutumika katika
kutayarisha mboji.

Aina za viazi vitamu
Kuna aina nyingi za viazi vitamu zinazolimwa ulimwenguni. Hapa nchini Tanzania aina
zinazolimwa zaidi ni Ukerewe, Simama, Kakamega, Karoti C, Mwananjemu, Ali mtumwa mayai, Mavuno, Pananzala, Kibakuli, Sinia,Vumilia na Polista

Uzalishaji
Zao hili hustawi maeneo mengi Nchini Tanzania. Viazi hustawi vizuri katika maeneo ya tambarare yenye udongo tifutifu, unaoruhusu maji kupenya kwa urahisi. Udongo wa mfinyazi na wenye kokoto nyingi haufai kwani huzuia mizizi kupenya na kupanuka.  Shamba jipya litayarishwe vizuri kwa kufyeka vichaka na kung’oa visiki. Majani yafukiwe wakati wa kutengeneza matuta ili kuongeza rutuba ya udongo.

Viazi vipandwe kwa kutumia Marando yenye urefu wa sentimita 30 kwa mavuno bora.
Inashauriwa kutumia sehemu ya juu ya shina kwa mavuno zaidi. Marando yapandwe katika umbali wa sentimita 25 hadi 30 kutoka mmea hadi mmea na sentimita 60 hadi 75 kutoka tuta hadi tuta.
Viazi pia vyaweza kupandwa kwa kutumia viazi vyenye afya vyenye uzito wa kati ya gramu
20 hadi 30. Hata hivyo inashauriwa kutumia marando ili kupata mavuno zaidi na kuepuka
kuenea kwa magonjwa.

Kutunza shamba
Ni muhimu kupalilia viazi vitamu katika miezi miwili ya mwanzo ili kuupa mmea nguvu ya
kutambaa vizuri. Baada ya muda huo, viazi huweza kufunika ardhi na hivyo huzuia uotaji wa
magugu. Viazi hushambuliwa na wadudu mbalimbali wakiwemo kipepeo, mbawa kavu, fukusi na minyoo fundo.Pia hushambuliwa na magonjwa yakiwemo magonjwa yanayotokana na virusi
kama Sweet Potato Chlorotic Stunt virus (SPCSV). Magonjwa na wadudu yaweza kudhibitiwa kwa kuzingatia usafi wa shamba, kubadilisha mazao, na kuzingatia udhibiti sango.

MATUMIZI YA MBOLEA ZA VIWANDANI NA
SAMADI
Samadi hutoa virutubisho kama vile N, P, K, Ca, Mg , S. Samadi ikitumiwa vizuri huchangia katika kuimarisha mazao, huboresha ubora wa udongo na hulinda unyevu unyevu. Weka samadi angalau siku 90 au 120 kabla ya kuvuna mazao yoyote ambayo yanaweza kuliwa bila kupikwa.
Virutubisho katika samadi katika tani 1:
Samadi za ng’ombe (32% DM): kg N 5.9, kg P 2.6 na kg K 5.4
Samadi za nguruwe (40% DM): kg N 8.2, kg P 5.5 na kg K 5.5
Samadi za kuku (57% DM): kg N 16.6, kg P 7.8 na K 8.8
Virutubisho/madini katika mfuko mmoja (kilo 50) cha 15-15-15 mbolea ambayo ina N kilo 7.5, P
kilo 3.3, na K kilo 6.2, kwa mtiririko.
Njia bora za matumizi ya samadi:
  1. Epuka kuweka samadi baada ya kupanda mazao
  2. Changanya samadi na udongo kabla ya kupanda
  3. Usitumie samadi ya mbwa au paka kwa sababu aina hizi kushiriki vimelea wengi na binadamu
Osha vizuri mazao yanayotoka katika shamba ambalo umetumia samadi kabla ya matumizi

Uvunaji
Viazi vitamu huwa tayari kuvunwa miezi mitatu hadi minne tangu kupanda kutegemea hali ya hewa. Viazi vinaweza kuvunwa kidogo kidogo kwa kutumia mikono, vijiti, jembe, au rato kadrivinavyohitajika. 

Aidha inashauriwa viazi visiachwe ardhini muda mrefu bila kuvunwa kwani vitakomaa sana na kuwa na nyuzi, na hivyo kuharibu ubora wake. Pia kuacha viazi muda mrefu hukaribisha mashambulizi ya wadudu kama fukusi na kuoza. Kwa maeneo makubwa zaidi, inashauriwa kutumia mashine ya kukokotwa na ng’ombe.

Uvunaji ufanywe kwa uangalifu ili kuhakikisha viazi visikatwekatwe wala kuchubuliwa wakati wa kuvuna. Mavuno ya viazi hutofautiana kulingana na aina,hali ya hewa, na udongo. Mavuno ya viazi yanakadiriwa kufikia tani 12 kwa ekari.

UCHAKATAJI
viazi vinachakatwa ili:
  • Vikae muda mrefu bila kuharibika
  • Kupunguza uwingi na kurahisisha usafirishaji
  • Kuondoa sumu katika viazi
  • Kutengeneza aina mbali mbali za vyakula zenye radha nzuri, hurufu na mwonekano nzuri
Kuzalisha malighafi ya viwanda
Kazi za uchakataji wa viazi
Kumenya: Karibu mazao yote ya viazi hutengenezwa kwa kumenywa kwanza. Kumenya
kunaongeza ubora na usalama wa chakula.
Ukamuaji: Njia za kienyeji za kukamua kwa mawemazito na magogo ni hatari, kazi ngumu na huchukua muda mrefu. Zipo mashine za kukamua kwa sasa

Ukaushaji: viazi hukaushwa kati ya 12 – 14% ya unyevu nyevu kabla kuhifadhi. Njia iliyozoeleka ya kienyeji ni kwa jua pia mashine.

Usagaji: viazi vyaweza kutengenezwa unga kabla ya matumizi ya nyumbani au viwandani
KILIMO BORA CHA VIAZI VITAMU KILIMO BORA CHA VIAZI VITAMU Reviewed by BENSON on November 12, 2017 Rating: 5

No comments