UFAHAMU UGONJWA MWINGINE AMBAO UNASUMBUA VIFANGA UNAITWA (CHICK PASTING).

Related image

Katika malezi ya vifaranga kumekuwa na tatizo sugu ambalo kwa bahati mbaya wafugaji wengi hawalijuhi na limekuwa likiwatesa sana. Vifaranga wadogo walio chini ya umri wa wiki moja wamekuwa na tatzo la kugandia kinyesi nje ya njia zao za haja yaani kwenye kale katundu kakutolea kinyesi. Wakati mwingine huziba njia ya choo na kumsababishia kifo kifaranga lakini hata asipokufa hukosa raha na mwishowe na ukuaji usiokuwa mzuri.

Kwa uzoefu wangu nimegundua kuwa zaidi 50% ya vifaranga wanaopata tatizo hilo ufa kama wasipopata huduma inayostahili. Mara nyingi unaweza kushangaa vifaranga wako wanakosa raha, wanakufa, nk. Lakini ukimchunguza vizur utamkuta na uchafu kwenye njia zake za kutolea haja kubwa na pengine pameziba kabsa.

Tatzo hili husababishwa na kuwapa chakula kingi vifaranga na kuwapa maji kidogo au usipate kabisa.Kifaranga anapozaliwa kama kiumbe mwingine huwa hajawa  imala katka maumbo yake ya mfumo wake wa mmeng'enyo hivyo unapompa chakula bila maji ya kutosha ni kwamba hata upataji wake wa choo itakuwa wa tabu.

Kuepuka hili tatzo unapaswa kuanzia siku moja hadi 5 kuhakikisha vifaranga wako wanapata maji mengi na chakula cha wastani ili kumuwezesha njia zake za mmengenyo kukaa sawa na kutoathirika na vitu vikavu na vigumu. Ili kuliwezesha hili kuepukana na kadhia hiyo. Pia natoa angalizo na fundisho kuwa, vifaranga wadogo hawawezi kujishughurisha sana kutafuta chakula na maji yalipo badala yake kinachokuwa mbele yake anakula na kama hakuna kitu basi sasa akikuta chakula bila maji tatzo linaanzia hapo.

Jinsi ya kuwahudumia walioathirika ni kuwasafisha kwa kutumia maji ya uvuguvugu au kitu chochote mithiri yake ili kuhakikisha unaondoa uchafu bila ya kumuumiza na njia yake ya haja ibaki safi.Wakati huo huo inapendekezwa ukiwa unampatia Antibacterial ili kumuepusha na madhara zaidi ya hayo na pia inashauriwa kuwa unampaka mafuta ya mgando asili ya jelly kwa ajili ya kumlainisha njia yake ya haja ili asiumie zaidi.
UFAHAMU UGONJWA MWINGINE AMBAO UNASUMBUA VIFANGA UNAITWA (CHICK PASTING). UFAHAMU UGONJWA MWINGINE AMBAO UNASUMBUA VIFANGA UNAITWA (CHICK PASTING). Reviewed by BENSON on November 15, 2017 Rating: 5

1 comment

  1. Je mbali nahii blog mnayo application naka mnayo inaitwaje? Hiliniweze kui download.

    ReplyDelete