UFAHAMU UGONJWA WA KUHARA DAMU ( COCCIDIOSISI) AMBAO HUWASHANBULIA KUKU KWA KIWANGO KIKUBWA.

Related image
Ugonjwa huu husababishwa na vimelea vya protozoa ambovyo ni jamii ya Eimeria acervulina. Vimelea hivi hupenda kuish ktk mazingira machafu,  kama vyakula vilivyooza,  na kwenye unyevunyevu na kinyesi.

Mara nyingi vifaranga huugua ugonjwa huu mara kwa mara kwa kula mavi yao na maji wanayomwagamwaga katik mabanda. Ugonjwa hutibika mara moja na pia dalili hujitokeza mapema sana ktk siku ya pili tangu maambukizi
.
Dalili za ugonjwa huu  
1. Kuku kushusha mbawa
2. Kinyesi cha damu au brown au vyote kwa pamoja
3. Kuku kupungia uzito. 

Kinga za ugonjwa huu
1. Mfugaji azingatie usafi wa mara kwa mara katika banda lake.
2. Pia kuku wadogo na wakubwa wakae tofaut ili kuepusha maambukizi.
3.Kwa kuwa ugonjwa huu uambatana na majimaji hakikisha banda linakuwa kavu na kuweka maji vizurikutomwagika mwagika. 
4.Piga chokaa mabanda yako mara kwa mara.  Weka viatu vya kuingia bandan mana unaweza kanyanga uchafu wa vimelea ukaingia nao bandani.
5. Sio lazima kila mgen kuingia bandani na hii hupunguza kasi ya maambukizi.

Tiba. 
Ugonjwa huu hutibika kirahic sana.  Na dawa zinazotibu ugonjwa huu ni dawa za sulphonamides
Mf,  esb3
       Amprolium
Zote kwa cku 5-7.

Muhimu: Watenge kuku wote wagonjwa na unapotibu tibu kuku wote kwa pamoja. 
UFAHAMU UGONJWA WA KUHARA DAMU ( COCCIDIOSISI) AMBAO HUWASHANBULIA KUKU KWA KIWANGO KIKUBWA.  UFAHAMU UGONJWA WA KUHARA DAMU ( COCCIDIOSISI) AMBAO HUWASHANBULIA KUKU KWA KIWANGO KIKUBWA. Reviewed by BENSON on November 16, 2017 Rating: 5

No comments