KAMA UNAFUGA KUKU NA HUNA UHAKIKA KAMA WALISHAKWISHA KUPEWA CHANJO FANYA YAFUATAYO.



Inawezekana kuku ambao unawafuga umewanunua au huna kumbukumbu kama walikwishapewa chanjo, kama ndivyo hivyo basi unachotakiwa kufanya kwa sasa ni njia hii.
Kwanza uwape kuku wako antibiotic ili kuwasaidia kuua magonjwa ya tumbo na mafua kama wanayo.

Hivyo basi anza kuwapa dawa kwa mtiririko huu na nitakueleza kwanini.
1. Wape dawa hizi mbili kwa maramoja kisha uchanganye na vitamin ya amin total.
A)Vitacox ya kepro uholanzi
B)Tylodox ya kepro uholanzi
C)Vitamin ya amin total

Dawa hizo hapo juu wape kwa maramoja yani uzichanganye Kwenye maji zote tatu kwa maramoja.

Dozi na vipimo
kama kuku wako wana uwezo wa kumaliza lita10 kwa siku basi weka vipimo hivi;
Weka maji Lita10, weka kijiko kimoja cha dawa ya Vitacox, kijiko kimoja cha dawa ya Tylodox na kijiko kimoja cha vitamin ya Amin Total. Changanya vizuri na uwape kuku wanywe siku nzima hayo maji yenye mchanganyo wa hizo dawa. Na unatakiwa kuwapa dozi hiyo kwa mfululizo wa siku5 bila kuvusha hata siku moja.

kijiko kinachotumika kupima dawa hapo ni kile kijiko cha chakula nasisitiza tumia kijiko cha chakula kila unachotumia kulia wali.

Kama kuku wako hawamalizi maji ya lita10 kwa siku basi weka maji lita5 na hapa unafata utaratibu huo huo kama hapo juu nilivyoeleza. Isipokuwa tu kijiko utakachotumia kwenye maji ya lita5 ni kijiko cha chai, kile kijiko kidogo kinachotumikaga kuwekea sukari kwenye chai kumbuka ni kile kidogo sio cha chakula.

Lakini vipimo ni hivyo hivyo unaweka kijiko kimoja kimoja cha kila dawa hapo tylodox kijiko kimoja, Vitacox kijiko kimoja na vitamin ya amin total kijiko kimoja. Siku ni zile zile 5 mfululizo na maji yaliyochamganywa yakae masaa24 (siku moja) kama hawajayamaliza mwaga na uchanganye tena mengine yakiisha kabla ya muda changanya mengine kwa vipimo hivyo hivyo

SABABU ZA KUWAPA KUKU HIZO ANTIBIOTICS
1. Tunawapa Kuku hizo antibiotics ili kusaidia kuondoa magonjwa ya tumbo na mfumo wa hewa (mafua na kifua) kama yapo kwa hao kuku kabla ya kuwapa chanjo. Na hii ni kwasababu kuku ukimpa chanjo wakati ana maambukizi ya magonjwa mengine mfano mafua,typhoid, kipindupindu, kuhara damu na mengine ataumwa na kufa badala ya kupona, kumbuka chanjo hupewa kuku mzima na sio magonjwa.

2. Baada ya kuku kumaliza dozi ya antibiotics kaa siku tatu bila kuwapa dawa yoyote yani baada ya kumaliza siku 5 tangu waanze hizo dawa za awali kaa siku tatu ya nne uwape dawa ya minyoo. Siku ya 9 uwape dawa ya minyoo.

3. Baada ya kuwapa dawa ya minyoo wakamaliza  kaa kwa muda wa siku 7 bila kuwapa dawa yoyote(wiki moja) Siku inayofuata baada ya wiki kupita ndio sasa uwape chanjo ya mdonde

5.Baada ya kuwapa chanjo ya mdonde unakaa tena wiki moja bila kuwapa dawa yoyote siku inayofuata unawapa *lchanjo ya gumboro


Ukimaliza mzunguko huo kuku wako watakuwa wapo salama kabisa ila utatakiwa kurudia chanjo kila baada ya miezi mitatu kupita
KAMA UNAFUGA KUKU NA HUNA UHAKIKA KAMA WALISHAKWISHA KUPEWA CHANJO FANYA YAFUATAYO. KAMA UNAFUGA KUKU NA HUNA UHAKIKA KAMA WALISHAKWISHA KUPEWA CHANJO FANYA YAFUATAYO. Reviewed by BENSON on November 18, 2017 Rating: 5

No comments