CANNIBALISM KWA KUKU NINI?

Image result for KUKU KUDONOANA

"Cannibalism,"

Kudonoana kwa kuku ni tatizo linalo wa sumbua wengi, ni moja ya athari ya lishe duni. Ni kisema lishe duni na maanisha chakula wanacho kula kukosa vurutubisho muhimu vya madini au kuku kutokula chakula cha kutosha. 

#Hizi ni moja ya sababu zinazo pelekea kuku kudonoana.

1.Kuku kukaa wengi kwenye eneo dogo

2. Tabia yao

3.Ubaguzi wa rangi
     
 Hii Mara nyingi hutokea kwa kuku weusi ukiwachanganya na kuku mweupe au rangi ingine tofauti, kuku weusi Mara nyingi huwa ni wakali sana Kwahiyo ukiona kuku bandani kwako kadonolewa chunguza kwa makini chanzo ninini! Kama ni ubaguzi wa rangi unaweza watenga hao weusi.
4. Kuku kutokupata chakula cha kutosha

5.Upungufu wa madini ( protini)

6. Kukosa kitu walicho kizoea au kuboreka

  Kwa mfano kuku ukiwazoesha kuwa changanyia Damu kwenye chakula , siku utakapo punguza kipimo au kuacha kabisa kuwa changanyia  damu  ambayo umewazoesha kuwa changanyia lazima watadonoana.

Kuku ukiwa zoesha kuwa fungia mchicha hasa wale kuanzia  mwezi mmoja hadi wa miezi 4  siku utakapo acha kuwafungia mchicha inaweza sababisha wakadonoana.

Kuku hupenda kuparuaparua na kuzunguka zunguka. Wakikosa nafasi na vitu vya kudonoa donoa huanza kudonoana wenyewe kwa wenyewe. 

7. Mwanga mkali 

8. Msongo
  Banda lenye joto sana na lisilo pitisha hewa vizuri huwapatia msongo/stress kuku, na kuku huweza kuanza kudonoana. 

9. Uhaba wa vyombo bandani👇

   Hii hutokana na kuwa na kuku wengi halafu vyombo vichache vya chakula , Kwahiyo wakati wa kula lazima watagombania na kudonoana

Kuku wa umri tofauti kuwekwa kwenye banda moja

#Tiba Kinga

#Tiba___ Tumia Protini (Amino Acid) stahiki kulingana na tatizo.
Mfano: (methionine , lysine nk)

#Kinga

_Changanya Proteni kiwango kizuri kwenye chakula cha kuku,chakula cha kuku kijumuishe virutubisho vyenye asili ya wanyama ambavyo ni chanzo kizuri cha Proteni

_Hakikisha kuku wako wanakaa kwenye eneo la kutosha . hii inategemea  aina ya kuku na umri wake.

_ Hakikisha kuku wako wana kula chakula na kushiba

_Banda la kuku wako liwe na hewa ya kutosha

_Usiweke kuku umri tofauti katika banda moja

_Uwe unatoa mizoga haraka bandani

_ Wafanye kuku wako wawe wenye furaha , kwa kuwawekea vifaa vya michezo  (bembea). 

Pia wafungie mchicha ili wawe bize na kuudonoa huo. Unaweza wafungia mchicha, kabeji nk



CANNIBALISM KWA KUKU NINI? CANNIBALISM KWA KUKU NINI? Reviewed by BENSON on February 02, 2018 Rating: 5

No comments