JINSI YA KUZUIA WADUDU NA MAGONJWA KATIKA ZAO LA BILINGANYA, sehemu ya 3

Image result for magonjwa ya bilinganya

Wadudu waharibifu
Vinyotomvu.
Wadudu waharibifu katika bilinganya hutambuliwa zaidi katika sehemu ya chini ya jani. Hufyonza utomvu wa majani na kusababisha majani kuwa na mabaka meupe au njano. Mashambulizi yakizidi majani huangauka chini. Vinyamtomvu wanaweza kuzuiwa kwa kunyunyizia moja ya dawa zifuatazo;
1.   Dimethoate
2.    Karate.

Vidukari.
Hawa ni wadudu wadodgo wenye rangi nyeusi. Hushambulia majani machanga na kuyasababishia huduma na kunjamana. Zuia wadudu hawa kwa kutumia dawa zifuatazo;
1.   Dimercon 50% E.C
Utitiri wa mimea.
Ni wadudu wadogo wenye rangi nyekundu iliyoiva. Hushambulia mmea kwa kufyoza mtomvu. Majani yakishambuliwa huonyesha utando kama wa buibui. Mashambulizi yakizidi mmea hudumaa, kukauka na hatimaye kufa. Njia ya kuzuia wadudu hawa ni kubadilisha mazao shambani. Kwa mfano mara baada ya kuvuana zao hili linalofuata liwe ni zao lingine. Pia dawa aina ya furadan inaweza kutumika kuzua wadudu hao.

Magonjwa.
Mnyauko backteria.
Ugonjwa huu husababishwa na bacteria. Mmea ulioshambuliwa hunyauka ghafla wakati wa jua kali. Unaweza kuzuia ugonjwa huu kwa kubadilisha mazao sahambani, na endapo kama ugonjwa huo utakuwa umekithiri  sana shambani unashauriwa usipande zao hilo la bilinganya kwa muda wa miaka mitatu hadi mitano. Au njia nyingine ni kupanda aina nyingine ya bilinganya ambayo nilieleza siku ya juzi.

Phomopsisi Vexans.
Ugonjwa huu husabaishwa na bacteria lakini pia hushambulia shina, majani na matunda yenyewe.

Verticillium wilt.
Husababuisha mmea kudumaa, majani kunjamana na kuanguka, jinsi ya kuzuia ugonjwa huu ni kung`oa mimea yote  iliyoshambuliwa kish kuichoma moto. Lakini pia inashauriwa shamba liwe safi muda wote.

Kuvuna bilinganya.
Zao hili huvunwa miezi miwili au mitatu tangu kupandikzwa kwake. Uvunaji hufanyika kwa muda wa miezi mine, lakini paia inashauriwa uvune bilinganya mara baada ya matunda kukomaa, kwani matunda yaliyokomaa sana hayafai kuliwa. Pia inasemakana kama matunzo yote yakazingatiwa shamba la hekta moja linauwezo wa kutoa tani 50/60.

ASANTE SANA KWA KUWA NASI HAPA KATIKA BLOG YETU YA KILIMO BORA,  AMBAPO KWA SIKU TATU MFULULIZO TULIKUWA TUNAJIFUNZA KUHUSU KILIMO BORA CHA BILINGANYA, TUKUTENE SIKU YA KESHO KWA SOMO JINGINE, ASANTE

JINSI YA KUZUIA WADUDU NA MAGONJWA KATIKA ZAO LA BILINGANYA, sehemu ya 3 JINSI YA KUZUIA WADUDU NA MAGONJWA KATIKA ZAO LA BILINGANYA, sehemu ya 3 Reviewed by BENSON on January 07, 2018 Rating: 5

No comments