JAMBO LA MUHIMU SANA UNALOTAKIWA KULIJUA KABLA YA KUANZA KUFUGA KUKU.

Picha inayohusiana

Unapotaka kujikita katika suala la ufugaji wa kuku ipo haja kubwa ya kuweza kufikiria ni kwanama gani utaweza kuwa mfugaji bora wa kuku, Hii ni kwa wote, wafugaji na wanaotaka kuanza kufuga. Unapotaka kuanza ufugaji unatakiwa uanze na ufugaji mdogo hata kama una mtaji mkubwa. Kwa kufanya hivi itakusaidia kupata uzoefu katika nyanja zifuatazo:



1.  Utunzaji.
Kwa kuanza na kiasi kidogo itakusaidia kujua ni ukubwa gani unafaa kwa kuku wangapi, ukiwa na kuku wangapi utalisha chakula kiasi gani, pia utapata uzoefu wa chanjo muhimu zinazohitajika hali ambayo itakurahisishia pindi utapoanza ufugaji mkubwa.

2. Soko
Hapa tunalenga upatikanaji wa wateja wa bidhaa zako za mifugo, itakusaidia kujua wateja waliopo wanavutiwa na bidhaa ya aina gani, kwa mfano mayai utajua wanapenda mayai ya kiini cheupe au cha njano? Kwa kufaham wanchokihitaji utajua ufanye nini ili ukidhi wanachokihitaji.

3. Changamoto
Ukianza na ufugaji mdogo pia itakusaidia kujua changamoto zilizopo kwenye ufugaji na utajifunza ni jinsi gani ya kuzitatua au kukabiliananazo kabla  ya kuanza ufugaji mkubwa.


Hivyo ni muhimu kuweza kuyazingatia hayo ili uweze kuwa mfugaji mwenye mfagaji mwenye mafanikio
JAMBO LA MUHIMU SANA UNALOTAKIWA KULIJUA KABLA YA KUANZA KUFUGA KUKU. JAMBO LA MUHIMU SANA UNALOTAKIWA KULIJUA KABLA YA KUANZA KUFUGA KUKU. Reviewed by BENSON on October 22, 2017 Rating: 5

No comments