KILIMO BORA CHA PARACHICHI

Tunda hili lina faida nyingi sana, mbali ya kutumika kama zao la kiuchumi lakini pia hutumika kuimarisha afya ya mwili

1. Faida za Parachichi upande wa Lishe

-Tunda lina vitamini zifuatazo

1. Lina Vitamini A-husaidia sana kuimarisha Macho kuona vizuri

2. Lina Vitamini B (B1-B12)- Husaidia sana mfumo wa misuli ya mwili kuwa sawasa na kuuepusha mwili na matatizo ya nerve

3. Lina Vitamini C-Husaidia sana upande wa kuimarisha ngozi, kwa sababu liko na mafuta, lina zaidi ya mara 4 ya virutubisho vya vitamini C vinavyopatikana katika machungwa

4. Lina vitamini D-ambapo husaidia sana kuimarisha mifupa ya mwili

5. Lina vitamini E-hii husaidia sana kuimarisha seli za uzazi, linasaidia sana kuongeza nguvu na utengenezwaji wa seli za uzazi

6. Lina vitamini K-Husaidia sana kuganda kwa damu, na kuongeza uzalishaji wa chembe hai nyekundu za damu

Madini- (Mineral Elements)
Ni tunda lenye

1. Madini ya Chuma kwa wingi (Fe)-Haya huaidia sana utengenezwaji wa damu, na kuongeza uwezekano wa damu kuwa na oxygeni ya kutosha na kusafirishwa kwa urahisi

2. Madini ya Calcium-Lina madini ya calcium, yanayosaidia kama ufanyaji wa kazi wa seli hai za mwili

3. Lina virutubisho vingine vidogo vidogo vingi, vinavyotakiwa katika ufanyaji kazi mzuri wa selli hai za mwili


2. Agronomy ya ParachichiHali ya hewa

-Ni tunda linalopenda sana sehemu za baridi, maeneo kama ya Rungwe-Mbeya, Njombe, Makete, linastawi vizuri sana, na huwa na Fatty Contenty kubwa

Joto

Nyuzi 15-25 Sentigrade

Muinuko
Mita 1200-1800 kutoka usawa wa baridi

Udongo
-Uwe kichanga tifutifu (Sandy loam), usiotuamisha maji

Aina za Parachichi
1. Zipo aina za kiasiliKila sehemu kuna iana za parachichi ambazo ni za asili ya eneo husika, parchichi hizi, huwa ndefu sana, na mavuno machache

2. Zipo aina za kisasa (Chotara)
Ziko aina nyingi sana za Parachichi chotara, na hizi hapa chini ni baadhi ya zile maarufu hapa tanzania

i. Hass
-Hii ni aina maarufu sana katika aina za parachichi



-Ni tunda linalokuwa na vipere vipere
-Limechongoka juu na chini
-Linahifadhika kwa urahisi

ii. Aina ya pili ni Fuerte
-Hili ni aina ya parachichi lenye ngozi laini saini, ngozi yake inateleza kama imepakwa mafuta
-liko na mafuta mengi ila linawahi kuoza
-Ni zuri kwa matumizi ya kawaida , si kwa kusafirisha umbali mrefu





-Aina hii ikilimwa sehemu za miinuko na baridi sana, inafaa sana kutoa mafuta mengi yanayoweza kutumika kutengeza lotion na baadhi ya vyakula vya mifugo

iii. Aina ya tatu maarufu hapa tanzania -inaitwa X-ikulu
-Ana hii ni maarufu sana kwa mikoa ya nyanda za juu kusini (Mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya na Ruvuma)
-Mti wa aina hii huwa na majani mapana kama mti wa embe
-Mti huu huchukua muda mrefu sana kustawi
-Tunda lake huwa ni kubwa, na lina gharama sana

UPandaji wa Parachichi

Nafasi kati ya shimo na shimo

-Umbali wa kutoka shimo hadi shimo ni MITA 7
-UMbali wa kutoka mstari hadi mstari ni MITA 7

Lakini kipimo hicho hapo juu kitategemea sana na aina ya udongo wa shamba lako , kwa udongo wenye Phosphorus kwa wingi (P), kipimo hicho hakifai, maana baada ya mika 3-5 miche ya mistari miwili inayofuatana itakuwa imekuatana katikati

-Hivyo nafasi yaweza kuwa

8M X 8M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 63 KWA EKA 1
AU 9M X 9M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 49 KWA EKA 1
AU 10M X 10M- KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 40 KWA EKA 1

Ukubwa wa shimo-Shimo laweza kuwa futi 2.5 x futi2.5 x futi 2.5 = (sm 75 x sm 75 x sm 75) (Kimo x upana x urefu)

-Au kipimo cha futi 3 x futi 3 x futi 3= sm 90 x sm 90 x sm 90

Mbolea

-Mbolea za kupandia zitakazohitajika , ni moja wapo kati ya hizi
-Samadi, Mboji, DAP, au TSP-Lakini ni muhimu kupandia mbolea asilia kama samadi ukachanganya kidogo na TSP au DAP

Kipimo cha mbolea,
-Kama ni mbolea za asili (Samadi au Mboji)-Kiasi cha kilo 16 hadi 20 kinapaswa kiwekwe katika shimo miezi 3 kabla ya kupanda mche

-Kama utapandia mbolea za viwandani (TSP, DAP, Minjingu, NPK etc)
kiasi cha gramu 100 hadi 200 kiwekwe kwa kila shimo, ichanganywe vizuri na udongo, kisha mmea uwekwe na kumwagiliwa

KUKOMAA NA KUTOA MAVUNO
-Parachichi hasa hizi za kisasa, hukomaa baada ya miezi 18 hadi 24

MAVUNO
-Kwa mara ya kwanza mti mmoja wa parachichi unaweza kukupa kati ya matunda 50 hadi 100 kwa mche mmoja.
-Mavuno hueongezeka kadri umri unavyoongezeka
-Mti wa parachichi ukifikia umri wa miaka 4 hadi 5, unakuwa full maturity, na hivyo mti mmoja unaweza kukupa hadi matunda 1200 kwa mwaka mzima '

FAIDA
kwa kipimo cha mita 10 x mita 10, katika eka mmoja utakuwa na mita 40
-Kila mti baada ya mika 5 unaweza kukupa wastani wa matunda 1000
-Hivyo kwa miti 40, utakuw na jumla ya matunda 40 x 1000= 40,000
-Kila tunda kwa bei ya shambani uuze tsh 250, na unamatunda 40,000
-Hivyo utapata jumla ya tsh 250 x matunda 40,000= 10,000,000tsh (MILIONI 10)

Magonjwa ya parachichi

Parcahichi kama mimea mingine inashambuliwa sana hasa upande wa majani pamoja na matunda
1. Yapo magonjwa ya majani, yanayosababishwa na fangasi/Ukungu, Algae, pamoja na wadudu, pamoja na lishe duni
Jani lililoshambuliwa na Alga


Mite-Utitiri mweupe Avocado lililoshambuliwa na Utitiri

2.Magonjwa ya matunda
Yasababishwayo na fangasi/Ukungu, Wadudu,na Lishe dunipia
-Tatizo la Athracnose husababishwa na Ukungu/Fangasi

-Tatizo la Scab, husababishwa na Ukungu/Fangasi hasa wakati wa baridi/unyevu mwingi

 
Thrips wa avocado Matunda yaliyoathiriwa na Thrips


DAWA
-Dawa za kutibu wadudu kama Karate, Matchi, Actellic 50 EC, za faa sana kumaliza wadudu katika mmea wa parachichi

-Dawa za Ukungu kama Ridomil Gold, Ebony 72 WP (Mancozeb na Metalaxyn), Ivory, na Nordox zaweza kutumika kumaliza matatizo ya ukungu

-Lishe ya mmea

Mbolea za kukuzia kama CAN, UREA NA SA (hasa kwenye maeneo yenye magadi kwa wingi, na chumvi nyingi) yaweza kutumika kubalane PH YA Udongo.

-Booster=Mbolea za majani, maua na matunda kama vile Polyfeed Starter, Polyfeed finisher, Wauxal macro mix, Potphos, au Multi K , Ni muhimu sana zikatumika wakati wa maua, na matunda ili kuzuia matunda ya parachichi kuabort (Fruit abortion) yakiwa machanga, pamoja na kuzuia matunda kudondoka yakiwa machanga.


Hitimisho
Parachichi-Kama matunda mengine, ukililima kitaalamu, na ukaweka juhudi na maarifa linakutoa katika umaskini
KILIMO BORA CHA PARACHICHI KILIMO BORA CHA PARACHICHI Reviewed by BENSON on January 18, 2018 Rating: 5

23 comments

  1. Unapochukua content kutoka ukurasa fulani wa website au blog nyingine, tafadhali aknowlege, otherwise huo ni wizi kama ulivyo wizi mwingine, chapisho lako loote umelikopi toka blog yangu http://kilimomaarifatajiri.blogspot.com/2015/10/kilimo-cha-parachichi-avocado.html , hilo ni chapisho la October 18 2015, wewe umechapisha la kwako wiki 2 tu zilizopita. Mimi ndiye kilimomaarifa.tajiri, na nina haki zote na chapishio hilo, Mambo mawili unayopaswa kufanya ni etheir uaknowledge hili chapisho kuwa umelitoa kwangu au Ufute kabisa, nakupa wiki moja kutekeleza hilo. Kabla ya kuliweka hilo chapisho katika blog yangu, nilikwisha uweka huo uzi katika uzi wangu uliopo jamii forums https://www.jamiiforums.com/threads/je-unataka-kulima-mazao-ya-mbogamboga-na-matunda-lakini-unakosa-maarifa-sahihi-karibu-tushauriane.929106/

    ReplyDelete
    Replies
    1. pole mkuu ndiyo mambo ya watanzania hayo

      Delete
    2. 😂😂😂😂 htal kweli fanya kaz ndugu

      Delete
  2. Nataka kuanza kilimo ila shamba sina mnanisaidiaje katika hilo???

    ReplyDelete
  3. ahsante sana kwa elimu hii... kwa yeyote anaetaka miche ya miparachichi naomba anitafute kwa mawasiliano hapo chini na BEI ZETU NI NAFUU KABISA. Pia tunatoa ushauri bureeee, pia tunatoa huduma ya upandaji kwa GHARAMA NAFUU(AFFORDABLE PRICE. chukua hatua utajirike na tuijenge Tanzania yetu.


    +255759 800 710 au
    mhanjemaurus933@gmail.com

    ReplyDelete
  4. HUU WIZI WA KUCHUKUWA KAZI YA MTU BILA HATA KUMSHUKURU SIO MZURI. INGAWA JAMBO LENYEWE LA KILIMO NI ZURI KWA KUWAELIMISHA WATU. NAMPONGEZA SANA http://kilimomaarifatajiri.blogspot.com KWA KUTUSAMBAZIA HILI JARIDA LIMETUPA MAARIFA JINSI YA KUENDELEA. UBARIKIWE SANA.

    ReplyDelete
  5. Kwa NJOMBE ni sehemu tu Ama NJOMBE yote?, inakubali Parachichi? Msaada tafadhari.

    ReplyDelete
  6. Nashukuru wa somo zuri la kilicho cha parachichi

    ReplyDelete
  7. Nahitaji parachichi grade A kwa ajili ya biashara... 0652309149

    ReplyDelete
  8. Niko Mkoa wa Simiyu naweza kuanzisha kilimo vha parachichi NASA kyk suala zima LA hali ya hewa?

    ReplyDelete
  9. Mashauri elimu ya kilimo Cha parachichi isifutwe Bali aliyechukua kazi hiyo na kuifanya Kama yake aweke wazi alikoitoa yaishe, elimu hiyo no mzuri Sana,ikifutwa watanzania wengi watakosa maarifa hayo.

    ReplyDelete
  10. Ukijua maana ya neno wizi kisheria pia neno haki miliki huwezi kujimilikisha Mali ya mtu kiholela, malizeni sitofahamu hiyo ili tupige hatua ya kupata makala za kilimo Cha zao Hilo.Msitunishiane misuli sisi tunaotarajia kupata elimu hiyo tutaikosa, hamuoni mtakuwa mmekosa upendo kwa watanzania masikini.Hekima itawale zaidi

    ReplyDelete
  11. Elimu hii bado inanitia moyo na kuamini kuwa kilimo kinauwezo wa kimtoa mtu kimaisha cha msingi ni kuthubutu tu!

    ReplyDelete
  12. Tupo njombe wauzaji was miche bora mkoani njombe pia tumekuwa washindi nyanda za juu kusini hao
    NEMES GREEN GARDEN
    Tunauza msimu wote miche IPO
    Tunatoa elimu yakilimo biashara
    Kilimo endelevu
    Namba 0755905323
    Tupi njombe kata ramadhan mtaa was maheve

    ReplyDelete
  13. Asante saaan kwa ushaur mzuri,ila mm nilikua natak Miche ya parachichi aina mbil Hass na X-ikulu mtanisaidiaj namba yangu ni 0621701032

    ReplyDelete
  14. Elimu nzuri sana. Tumashukuru sana. Naamini ntaifanyia kazi

    ReplyDelete
  15. Nina shamba nipo Arusha jinsi gan yakujua Miche na jinsi yakutunza

    ReplyDelete